‏ Psalms 142

Maombi Ya Kuokolewa Dhidi Ya Watesi

Utenzi wa Daudi. Alipokuwa pangoni. Maombi.

1 aNamlilia Bwana kwa sauti,
nainua sauti yangu kwa Bwana anihurumie.
2 bNamimina malalamiko yangu mbele zake,
mbele zake naeleza shida zangu.

3 cWakati roho yangu inapozimia ndani yangu,
wewe ndiwe unajua njia zangu.
Katika njia ninayopita
watu wameniwekea mtego.
4 dTazama kuume kwangu na uone,
hakuna hata mmoja anayejihusisha nami.
Sina kimbilio,
hakuna anayejali maisha yangu.

5 eEe Bwana, nakulilia wewe,
nasema, “Wewe ni kimbilio langu,
fungu langu katika nchi ya walio hai.”
6 fSikiliza kilio changu,
kwa sababu mimi ni mhitaji sana;
niokoe na wale wanaonifuatilia,
kwa kuwa wamenizidi nguvu.
7 gNifungue kutoka kifungo changu,
ili niweze kulisifu jina lako.

Ndipo wenye haki watanizunguka,
kwa sababu ya wema wako kwangu.
Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.