‏ Psalms 101

Ahadi Ya Kuishi Kwa Uadilifu Na Kwa Haki

Zaburi ya Daudi.

1 aNitaimba juu ya upendo wako na haki yako;
kwako wewe, Ee Bwana, nitaimba sifa.
2 bNitazingatia kuishi maisha yasiyo na lawama:
utakuja kwangu lini?

Nitatembea nyumbani mwangu
kwa moyo usio na lawama.
3 cSitaweka mbele ya macho yangu
kitu kiovu.

Ninayachukia matendo ya watu wasio na imani;
hawatashikamana nami.
4 dMoyo wa ukaidi utakuwa mbali nami;
nitajitenga na kila ubaya.

5 eKila amsingiziaye jirani yake kwa siri,
huyo nitamnyamazisha;
mwenye macho ya dharau na moyo wa kiburi
huyo sitamvumilia.

6 fMacho yangu yatawaelekea waaminifu katika nchi,
ili waweze kuishi pamoja nami;
yeye ambaye moyo wake hauna lawama
atanitumikia.

7Mdanganyifu hatakaa
nyumbani mwangu,
yeye asemaye kwa uongo
hatasimama mbele yangu.

8 gKila asubuhi nitawanyamazisha
waovu wote katika nchi;
nitamkatilia mbali kila mtenda mabaya
kutoka mji wa Bwana.
Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.