‏ Psalms 113

Kumsifu Bwana Kwa Wema Wake

1 aMsifuni Bwana.

Enyi watumishi wa Bwana msifuni,
lisifuni jina la Bwana.
2 bJina la Bwana na lisifiwe,
sasa na hata milele.
3 cKuanzia mawio ya jua hadi machweo yake,
jina la Bwana linapaswa kusifiwa.

4 d Bwana ametukuka juu ya mataifa yote,
utukufu wake juu ya mbingu.
5 eNi nani aliye kama Bwana Mungu wetu,
Yeye ambaye ameketi juu kwenye kiti cha enzi,
6 fambaye huinama atazame chini
aone mbingu na nchi?

7 gHuwainua maskini kutoka mavumbini,
na kuwanyanyua wahitaji kutoka kwenye jalala,
8 hhuwaketisha pamoja na wakuu,
pamoja na wakuu wa watu wake.
9 iHumjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake,
akiwa mama watoto mwenye furaha.

Msifuni Bwana.
Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.

Everyone uses cookies. We do too! Cookies are little bits of information stored on your computer which help us give you a better experience. You can find out more by reading the STEPBible cookie policy.