‏ Psalms 125

Usalama Wa Watu Wa Mungu

Wimbo wa kwenda juu.

1 aWale wamtumainio Bwana ni kama mlima Sayuni,
ambao hauwezi kutikisika, bali wadumu milele.
2 bKama milima inavyozunguka Yerusalemu,
ndivyo Bwana anavyowazunguka watu wake
sasa na hata milele.

3 cFimbo ya waovu haitadumu juu ya nchi
waliopewa wenye haki,
ili wenye haki wasije wakatumia
mikono yao kutenda ubaya.

4 dEe Bwana, watendee mema walio wema,
wale walio wanyofu wa moyo.
5 eBali wale wanaogeukia njia zilizopotoka,
Bwana atawafukuza pamoja na watenda mabaya.

Amani iwe juu ya Israeli.
Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.