‏ Psalms 130

Kuomba Msaada

Wimbo wa kwenda juu.

1 aKutoka vilindini ninakulilia, Ee Bwana.
2 bEe Bwana, sikia sauti yangu.
Masikio yako na yawe masikivu
kwa kilio changu unihurumie.

3 cKama wewe, Ee Bwana, ungeweka kumbukumbu ya dhambi,
Ee Bwana, ni nani angeliweza kusimama?
4 dLakini kwako kuna msamaha,
kwa hiyo wewe unaogopwa.

5 eNamngojea Bwana, nafsi yangu inangojea,
katika neno lake naweka tumaini langu.
6 fNafsi yangu inamngojea Bwana
kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi,
naam, kuliko walinzi
waingojeavyo asubuhi.

7 gEe Israeli, mtumaini Bwana,
maana kwa Bwana kuna upendo usiokoma,
na kwake kuna ukombozi kamili.
8 hYeye mwenyewe ataikomboa Israeli
kutoka dhambi zao zote.
Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.