‏ Psalms 131

Kumtegemea Mungu Kwa Unyenyekevu

Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi.

1 aMoyo wangu hauna kiburi, Ee Bwana,
macho yangu hayajivuni;
sijishughulishi na mambo makuu kunizidi
wala mambo ya ajabu mno kwangu.
2 bLakini nimetuliza na kunyamazisha nafsi yangu;
kama mtoto aliyeachishwa kunyonya na mama yake,
kama mtoto aliyeachishwa kunyonya
ndivyo ilivyo nafsi iliyoko ndani yangu.

3 cEe Israeli, mtumaini Bwana
tangu sasa na hata milele.
Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.