‏ Psalms 16

Sala Ya Matumaini

Utenzi wa Daudi.

1 aEe Mungu, uniweke salama,
kwa maana kwako nimekimbilia.

2 bNilimwambia Bwana, “Wewe ndiwe Bwana wangu;
pasipo wewe sina jambo jema.”
3 cKwa habari ya watakatifu walioko duniani,
ndio walio wa fahari ambao ninapendezwa nao.
4 dHuzuni itaongezeka kwa wale
wanaokimbilia miungu mingine.
Sitazimimina sadaka zao za damu
au kutaja majina yao midomoni mwangu.

5 e Bwana umeniwekea fungu langu na kikombe changu;
umeyafanya mambo yangu yote yawe salama.
6 fAlama za mipaka zimeniangukia mahali pazuri,
hakika nimepata urithi mzuri.

7 gNitamsifu Bwana ambaye hunishauri,
hata wakati wa usiku moyo wangu hunifundisha.
8 h iNimemweka Bwana mbele yangu daima.
Kwa sababu yuko mkono wangu wa kuume,
sitatikisika.

9 jKwa hiyo moyo wangu unafurahia, na ulimi wangu unashangilia;
mwili wangu nao utapumzika salama,
10 kkwa maana hutaniacha kaburini,
wala hutamwacha Mtakatifu Wako kuona uharibifu.
11 lUmenijulisha njia ya uzima;
utanijaza na furaha mbele zako,
pamoja na furaha za milele
katika mkono wako wa kuume.
Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.

Everyone uses cookies. We do too! Cookies are little bits of information stored on your computer which help us give you a better experience. You can find out more by reading the STEPBible cookie policy.