‏ Psalms 23

Bwana Mchungaji Wetu

Zaburi ya Daudi.

1 a Bwana ndiye mchungaji wangu,
sitapungukiwa na kitu.
2 bHunilaza katika malisho
ya majani mabichi,
kando ya maji matulivu huniongoza,
3 chunihuisha nafsi yangu.
Huniongoza katika njia za haki
kwa ajili ya jina lake.
4 dHata kama nikipita katikati
ya bonde la uvuli wa mauti,
sitaogopa mabaya,
kwa maana wewe upo pamoja nami;
fimbo yako na mkongojo wako
vyanifariji.

5 eWaandaa meza mbele yangu
machoni pa adui zangu.
Umenipaka mafuta kichwani pangu,
kikombe changu kinafurika.
6 fHakika wema na upendo vitanifuata
siku zote za maisha yangu,
nami nitakaa nyumbani mwa Bwana
milele.
Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.