‏ Psalms 53

Uovu Wa Wanadamu

(Zaburi 14)

Kwa mwimbishaji. Mtindo wa mahalathi. Utenzi wa Daudi.

1 aMpumbavu anasema moyoni mwake,
“Hakuna Mungu.”
Wameharibika, na njia zao ni za uovu kabisa,
hakuna hata mmoja atendaye mema.

2 bMungu anawachungulia wanadamu chini
kutoka mbinguni
aone kama wako wenye akili,
wowote wanaomtafuta Mungu.
3 cKila mmoja amegeukia mbali,
wameharibika wote pamoja,
hakuna atendaye mema.
Naam, hakuna hata mmoja!

4 dJe, watendao mabaya kamwe hawatajifunza:
wale ambao huwala watu wangu
kama watu walavyo mkate,
hao ambao hawamwiti Mungu?
5 eHapo waliingiwa na hofu kuu,
ambapo hapakuwa cha kutetemesha.
Mungu alitawanya mifupa ya wale waliokushambulia;
uliwaaibisha, kwa sababu Mungu aliwadharau.

6Laiti wokovu wa Israeli ungalikuja kutoka Sayuni!
Wakati Mungu arejeshapo wafungwa wa watu wake,
Yakobo na ashangilie, Israeli na afurahi!
Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.