‏ Psalms 8

Utukufu Wa Mungu Na Heshima Ya Mwanadamu

Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya Daudi.

1 aEe Bwana, Bwana wetu,
tazama jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote!

Umeuweka utukufu wako
juu ya mbingu.
2 bMidomoni mwa watoto wachanga na wanyonyao
umeamuru sifa,
kwa sababu ya watesi wako,
kumnyamazisha adui na mlipiza kisasi.

3 cNikiziangalia mbingu zako,
kazi ya vidole vyako,
mwezi na nyota,
ulizoziratibisha,
4 dmwanadamu ni kitu gani hata unamfikiria,
binadamu ni nani hata unamjali?
5 eUmemfanya chini kidogo kuliko viumbe wa mbinguni,
ukamvika taji ya utukufu na heshima.

6 fUmemfanya mtawala juu ya kazi za mikono yako;
umeweka vitu vyote chini ya miguu yake.
7 gMifugo na makundi yote pia,
naam, na wanyama wa kondeni,
8 hndege wa angani na samaki wa baharini,
naam, kila kiogeleacho katika njia za bahari.

9 iEe Bwana, Bwana wetu,
tazama jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote!
Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.