‏ Matthew 22:41-45

Swali Kuhusu Mwana Wa Daudi

(Marko 12:35-37; Luka 20:41-44)

41 aWakati Mafarisayo walikuwa wamekusanyika pamoja, Yesu akawauliza, 42 b“Mnaonaje kuhusu Kristo?
Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta.
Yeye ni mwana wa nani?”

Wakamjibu, “Yeye ni mwana wa Daudi.”

43Akawaambia, “Inakuwaje basi kwamba Daudi, akinena kwa kuongozwa na Roho, anamwita Kristo ‘Bwana’? Kwa maana asema,

44 d “ ‘Bwana alimwambia Bwana wangu:
“Keti mkono wangu wa kuume,
hadi nitakapowaweka adui zako
chini ya miguu yako.” ’
45 Kama basi Daudi anamwita yeye ‘Bwana,’ awezaje kuwa mwanawe?”
Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.

Everyone uses cookies. We do too! Cookies are little bits of information stored on your computer which help us give you a better experience. You can find out more by reading the STEPBible cookie policy.