‏ Psalms 98

Mungu Mtawala Wa Dunia

Zaburi.

1 aMwimbieni Bwana wimbo mpya,
kwa maana ametenda mambo ya ajabu;
kitanga chake cha kuume na mkono wake mtakatifu
umemfanyia wokovu.
2 b Bwana ameufanya wokovu wake ujulikane
na amedhihirisha haki yake kwa mataifa.
3 cAmeukumbuka upendo wake
na uaminifu wake kwa nyumba ya Israeli;
miisho yote ya dunia imeuona
wokovu wa Mungu wetu.

4 dMpigieni Bwana kelele za shangwe, dunia yote,
ipaze sauti kwa nyimbo za shangwe na vinanda;
5 emwimbieni Bwana kwa kinubi,
kwa kinubi na sauti za kuimba,
6 fkwa tarumbeta na mvumo wa baragumu za pembe za kondoo dume:
shangilieni kwa furaha mbele za Bwana, aliye Mfalme.

7 gBahari na ivume na kila kiliomo ndani yake,
dunia na wote wakaao ndani yake.
8 hMito na ipige makofi,
milima na iimbe pamoja kwa furaha,
9 ivyote na viimbe mbele za Bwana,
kwa maana yuaja kuhukumu dunia.
Atahukumu dunia kwa haki
na mataifa kwa haki.
Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.

Everyone uses cookies. We do too! Cookies are little bits of information stored on your computer which help us give you a better experience. You can find out more by reading the STEPBible cookie policy.