Psalms 89
Wimbo Wakati Wa Taabu Ya Kitaifa
Utenzi wa Ethani Mwezrahi.
1 aNitaimba juu ya upendo mkuu wa Bwana milele;kwa kinywa changu nitajulisha uaminifu wako
ujulikane kwa vizazi vyote.
2 bNitatangaza kuwa upendo wako unasimama imara milele
na uaminifu wako umeuthibitisha mbinguni.
3 cUlisema, “Nimefanya agano na mteule wangu,
nimemwapia mtumishi wangu Daudi,
4 d‘Nitaimarisha uzao wako milele
na kudumisha ufalme wako kwa vizazi vyote.’ ”
5 eEe Bwana, mbingu zinayasifu maajabu yako,
uaminifu wako pia katika kusanyiko la watakatifu.
6 fKwa kuwa ni nani katika mbingu
anayeweza kulinganishwa na Bwana?
Ni nani miongoni mwa viumbe vya mbinguni
aliye kama Bwana?
7 gKatika kusanyiko la watakatifu, Mungu huogopwa sana,
anahofiwa kuliko wote wanaomzunguka.
8 hEe Bwana Mwenye Nguvu Zote,
ni nani aliye kama wewe?
Ee Bwana, wewe ni mwenye nguvu,
na uaminifu wako unakuzunguka.
9 iWewe unatawala bahari yenye msukosuko;
wakati mawimbi yake yanapoinuka, wewe unayatuliza.
10 jWewe ulimponda Rahabu ▼
▼Rahabu hapa ina maana jina la Misri kwa fumbo, yaani mwenye majivuno (lakini sio Rahabu wa Yos 2).
kama mmojawapo wa waliochinjwa;
kwa mkono wako wenye nguvu,
uliwatawanya adui zako.
11 lMbingu ni zako, nayo nchi pia ni yako,
uliuwekea ulimwengu msingi
pamoja na vyote vilivyomo.
12 mUliumba kaskazini na kusini;
Tabori na Hermoni wanaliimbia jina lako kwa furaha.
13 nMkono wako umejaa uwezo;
mkono wako una nguvu,
mkono wako wa kuume umetukuzwa.
14 oHaki na hukumu ndio msingi wa kiti chako cha enzi;
upendo na uaminifu vinakutangulia.
15 pHeri ni wale ambao wamejifunza kukusifu kwa shangwe,
wanaotembea katika mwanga
wa uwepo wako, Ee Bwana.
16 qWanashangilia katika jina lako mchana kutwa,
wanafurahi katika haki yako.
17 rKwa kuwa wewe ni utukufu na nguvu yao,
kwa wema wako unatukuza pembe ▼
▼Pembe inawakilisha nguvu.
yetu.18 tNaam, ngao yetu ni mali ya Bwana,
na mfalme wetu mali ya Aliye Mtakatifu wa Israeli.
19Ulizungumza wakati fulani katika maono,
kwa watu wako waaminifu, ukasema:
“Nimeweka nguvu kwa shujaa,
nimemwinua kijana miongoni mwa watu.
20 uNimemwona Daudi, mtumishi wangu,
na nimemtia mafuta yangu matakatifu.
21 vKitanga changu kitamtegemeza,
hakika mkono wangu utamtia nguvu.
22 wHakuna adui atakayemtoza ushuru,
hakuna mtu mwovu atakayemwonea.
23 xNitawaponda adui zake mbele zake
na kuwaangamiza watesi wake.
24 yUpendo wangu mkamilifu utakuwa pamoja naye,
kwa Jina langu pembe yake itatukuzwa.
25 zNitauweka mkono wake juu ya bahari,
mkono wake wa kuume juu ya mito.
26 aaNaye ataniita kwa sauti, ‘Wewe ni Baba yangu,
Mungu wangu, Mwamba na Mwokozi wangu.’
27 abNitamteua pia awe mzaliwa wangu wa kwanza,
aliyetukuka kuliko wafalme wote wa dunia.
28 acNitadumisha upendo wangu kwake milele,
na agano langu naye litakuwa imara.
29 adNitaudumisha uzao wake milele,
kiti chake cha enzi kama mbingu zinavyodumu.
30 ae“Kama wanae wataacha amri yangu
na wasifuate sheria zangu,
31kama wakihalifu maagizo yangu
na kutoshika amri zangu,
32 afnitaadhibu dhambi yao kwa fimbo,
uovu wao kwa kuwapiga,
33 aglakini sitauondoa upendo wangu kwake,
wala sitausaliti uaminifu wangu kamwe.
34 ahMimi sitavunja agano langu
wala sitabadili lile ambalo midomo yangu imelitamka.
35 aiMara moja na kwa milele, nimeapa kwa utakatifu wangu,
nami sitamdanganya Daudi:
36 ajkwamba uzao wake utaendelea milele,
na kiti chake cha enzi kitadumu mbele zangu kama jua;
37 akkitaimarishwa milele kama mwezi,
shahidi mwaminifu angani.”
38 alLakini wewe umemkataa, umemdharau,
umemkasirikia sana mpakwa mafuta wako.
39 amUmelikana agano lako na mtumishi wako,
na umeinajisi taji yake mavumbini.
40 anUmebomoa kuta zake zote,
na ngome zake zote umezifanya kuwa magofu.
41 aoWote wapitao karibu wamemnyangʼanya mali zake;
amekuwa dharau kwa jirani zake.
42 apUmeutukuza mkono wa kuume wa adui zake,
umewafanya watesi wake wote washangilie.
43 aqUmegeuza makali ya upanga wake,
na hukumpa msaada katika vita.
44Umeikomesha fahari yake,
na kukiangusha kiti chake cha enzi.
45 arUmezifupisha siku za ujana wake,
umemfunika kwa vazi la aibu.
46 asHata lini, Ee Bwana? Utajificha milele?
Ghadhabu yako itawaka kama moto hata lini?
47 atKumbuka jinsi maisha yangu yanavyopita haraka.
Ni kwa ubatili kiasi gani umemuumba mwanadamu!
48 auNi mtu gani awezaye kuishi na asione kifo,
au kujiokoa mwenyewe kutoka nguvu za kaburi? ▼
▼Kaburi hapa maana yake ni Kuzimu, kwa Kiebrania ni Sheol.
49 awEe Bwana, uko wapi upendo wako mkuu wa mwanzoni,
ambao katika uaminifu wako ulimwapia Daudi?
50 axBwana kumbuka jinsi mtumishi wako amesimangwa,
jinsi ninavyovumilia moyoni mwangu dhihaka za mataifa yote,
51 aydhihaka ambazo kwazo adui zako
wamenisimanga, Ee Bwana,
ambazo kwazo wamesimanga
kila hatua ya mpakwa mafuta wako.
52 azMsifuni Bwana milele!
Amen na Amen.
Copyright information for
SwhNEN
Welcome to STEP Bible
A simplified search is now available!Here are the frequently asked questions:
How do I read passages in Bibles?
- How do I look up a passage?
- How do I see three Bibles at once?
- How do I find a parallel gospel passage?
- How do I follow a Bible reading plan?
- How do I also see a commentary?
1) Click the Resource icon.
2) Click the resource for parallel gospel passage
2) Click the resource for parallel gospel passage
1) Click the Resource icon.
2) Plans for 1/2/3 years, chronological, Jewish etc
2) Plans for 1/2/3 years, chronological, Jewish etc
1) Click the Bible button.
2) Click on Commentaries
2) Click on Commentaries
How do I find words and phrases?
- How do I find words or topics?
- How do I search only some books in the Bible?
- How do I find a Greek or Hebrew word?
- How do I find a word only where it relates to a topic?
- How do I find more about search?
Video guide
1) Click on the search button
2) Click on Range
3) Select the books that you wish to search
1) Click on the search button
2) Click on Range
3) Select the books that you wish to search
Video guide
1) Click on the search button
2) Click on the Hebrew or Greek tab
3) Type in the Greek/Hebrew word in the search box, press Return, and wait for the table to fill itself.
4) View corresponding row to see Greek/Hebrew translation of the word
1) Click on the search button
2) Click on the Hebrew or Greek tab
3) Type in the Greek/Hebrew word in the search box, press Return, and wait for the table to fill itself.
4) View corresponding row to see Greek/Hebrew translation of the word
Video guide
1) Click on the search button
2) Click on the English tab
3) Type in the topic in the search box, press Return, and wait for the table to fill itself.
4) Click on one of the words or topics listed
1) Click on the search button
2) Click on the English tab
3) Type in the topic in the search box, press Return, and wait for the table to fill itself.
4) Click on one of the words or topics listed
How do I do a word study?
- What information can I find about a word?
- Meaning: how the word is used throughout the Bible
- Dictionary: academic details about the word
- Related words: similar in meaning or origin
- Grammar: (only available for some Bibles)
- Why do only some Bibles have clickable words?
- What does “~20x” or “Frequency” mean?
- Why do some words have dropdown next to the frequency number?
- Where do I find the maps?
- How do I get the word frequency for a chapter or a book?
When you click on a word, the detailed lexicon opens with:
'Vocabulary' Bibles link the translation to Greek & Hebrew. So far, only some Bibles have this vocabulary feature. They are shown in the Bible select screen with the letter 'V'.
It is the number of occurrences of a word in the Bible. Click on it to see them all in the selected Bible(s).
This reveals different forms for some words and names. These details are often interesting to scholars, eg the word 'beginning' in Genesis.
Video guide
1st method:
Click on a place name then on the Map button in the detailed lexicon.
2nd method:
1) Click the Resource icon.
2) Click on "Places in the Bible"
1st method:
Click on a place name then on the Map button in the detailed lexicon.
2nd method:
1) Click the Resource icon.
2) Click on "Places in the Bible"
Video guide
1) Click on the analysis icon.
2) Click on the "Selected passage" button if no analysis is shown.
1) Click on the analysis icon.
2) Click on the "Selected passage" button if no analysis is shown.
How do I find more information on original languages?
- How do I see Greek/Hebrew vocabulary for my Bible?
- How do I see Greek/Hebrew transliteration for my Bible?
- How do I see Greek/Hebrew vocabulary for a verse?
- How can I view multiple Bibles together as an Interlinear?
- How do I see the various versions of the Greek OT?
- How do I display the color-coded grammar?
Video guide
1) Click on the Bible translation button
2) Refer to the legend and select the Bible translations with the Vocab feature
3) Click on the Option button, then click "Interlinear options”, then select "Greek / Hebrew". Original language vocab will be shown.
1) Click on the Bible translation button
2) Refer to the legend and select the Bible translations with the Vocab feature
3) Click on the Option button, then click "Interlinear options”, then select "Greek / Hebrew". Original language vocab will be shown.
Video guide
1) Click on the Bible translation button
2) Refer to the legend and select the Bible translations with the Vocab feature
3) Click on the Option button, then click "Interlinear options”, then select "Transliteration".
1) Click on the Bible translation button
2) Refer to the legend and select the Bible translations with the Vocab feature
3) Click on the Option button, then click "Interlinear options”, then select "Transliteration".
Video guide
1) Click on the verse number to list the words and meanings
2) Hover over or click on a word for more details about the word
1) Click on the verse number to list the words and meanings
2) Hover over or click on a word for more details about the word
Video guides
1) Click on the Bible translation button
2) Refer to the legend and select two Bible with the vocabulary feature
3) Click on the Option button, then click Interlinear”. Interlinear will be shown.
1) Click on the Bible translation button
2) Refer to the legend and select two Bible with the vocabulary feature
3) Click on the Option button, then click Interlinear”. Interlinear will be shown.
1) Click on the Bible translation button
2) Select “Ancient” for the language
3) Scroll down to see the Greek OT translations
Examples
2) Select “Ancient” for the language
3) Scroll down to see the Greek OT translations
Examples
Video guide
1) Click on the Bible translation button
2) Refer to the legend and select the Bible translations with the grammar feature
3) Click on "G" or "Grammar" at the navigation bar. The text will then be color coded.
Examples
1) Click on the Bible translation button
2) Refer to the legend and select the Bible translations with the grammar feature
3) Click on "G" or "Grammar" at the navigation bar. The text will then be color coded.
Examples
© STEPBible - 2024